1 Mei 2025 - 21:04
Kuimarishwa kwa uhusiano wa kibiashara kati ya Iran na Afrika / Isfahan kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika

Waziri wa Viwanda wa Mali, katika hafla ya kufunga Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji wa pamoja katika nyanja mbalimbali. Alieleza matumaini kwamba mkutano huu utasababisha mshikamano na maingiliano yenye tija kati ya pande hizo mbili, na akatambua kuwa sekta binafsi ina nafasi muhimu katika mchakato huu.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) — ABNA — Moussa Diallo, Waziri wa Viwanda, Madini na Biashara wa nchi ya Mali, leo Alhamisi tarehe 1 Mei, 2025 katika hafla ya kufunga Mkutano wa Tatu wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika uliofanyika Isfahan, alisema:

Mkutano huu umetuwezesha kuanzisha mahusiano na ushirikiano wa kibiashara kati ya Iran na Afrika katika nyanja mbalimbali kama kilimo, nishati, madini, afya, teknolojia, na nyinginezo.”

Akaongeza kuwa: “Tunatarajia uhusiano huu kuongezeka kwa ajili ya kuimarisha mshikamano, na mkutano huu umetufikisha katika hatua hiyo. Nina hakika mshikamano huu ni wa lazima.”

Waziri huyo alisema zaidi: “Mkutano huu si tu umetuwezesha kuimarisha uwekezaji wetu, bali pia umechangia kukuza mauzo ya bidhaa nje ya nchi. Kupitia vyumba vya biashara, uhusiano mzuri umeanzishwa kati ya sekta binafsi ya pande zote mbili, na ni lazima kusisitiza kuwa sekta binafsi ina mchango mkubwa katika maendeleo haya.”

Diallo alihitimisha kwa kusema: “Tuna matumaini makubwa kwa uhusiano tuliouanzisha, na kwamba uhusiano huu utazaa matunda. Tunatumaini uchumi kati ya Iran na Afrika utaendelea kuwa hai na wenye kasi.”

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha